Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, May 22, 2014

Hitilafu zashadidi kati ya Kongo Brazzaville na DRC

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewataka raia wote wa Jamhuri ya Kongo Brazzaville watakaoingia nchini humo, wawe na viza  na hati ya kusafiria. Richard Muyej Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa, hatua hiyo imechukuliwa ili kukabiliana na hatua zisizo za kibinadamu zilizoonyeshwa hivi karibuni na vikosi vya usalama vya Kongo Brazzaville za kuwafukuza raia wa Kongo Kinshasa nchini humo. Imeelezwa kuwa, uhusiano wa pande hizo mbili umeingia dosari baada ya serikali ya Kongo Brazzaville kuwafukuza raia wa Kikongo walioko nchini humo.
Shirika la Kimataifa la Wahajiri limetangaza kuwa, tokea kuanza operesheni ya kufukuzwa raia wa Kikongo kutoka nchini Kongo Brazzaville mwezi uliopita, zaidi ya Wakongo elfu 80 wamesharudishwa makwao. Inafaa kuashiria hapa kuwa, mwanzoni mwa mwezi uliopita, Polisi ya Kongo Brazzaville iliwafukuza wahajiri wa Kikongo wasiokuwa na vibali vya kuishi nchini humo kwa kisingizio cha kukabiliana na ongezeko la vitendo vya uhalifu na jinai. Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ina jumla ya watu milioni 76 huku Jamhuri ya Kongo Brazzaville ikiwa na jumla ya watu milioni  4 tu.

No comments: