Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 24, 2014

Waasi na serikali Mali wafikia makubaliano ya amani

Rais Mohamed Ould Abdel Aziz wa Mauritania na ambaye pia ni Mwenyekiti wa hivi sasa wa Umoja wa Afrika amefanikiwa kuzipatanisha pande hasimu nchini Mali. Makubaliano hayo yalifikiwa jana ambapo pande hizo zimekubaliana kuweka chini silaha na kufuata mwenendo wa amani nchini Mali. Rais Mohamed Ould Abdel Aziz wa Mauritania amesema kuwa, makubaliano hayo yamefikiwa baada ya mazungumzo kati ya maafisa wa AU na wawakilishi wa serikali ya Mali na wale waasi wa kaskazini mwa nchi hiyo. Kwa mujibu wa makubaliano hayo pande mbili zimeahidi kukomesha mapigano na kujiepusha kuendesha harakati zao katika nchi nyingine za jirani.
Tangu siku ya Jumamosi iliyopita, mji wa Kidal, umekuwa ukishuhudia mapigano ya hapa na pale kati ya pande mbili baada ya waasi wa Tuareg kuudhibiti mji huo. Kwa mujibu wa ripoti rasmi, karibu askari 20 wa serikali wameuawa huku wengine 30 wakijeruhiwa. Weledi wa mambo wanaitaja Ufaransa kuwa inahusika na mapigano hayo, ambayo ni njia moja wapo ya kuendelea kubakisha askari wake ndani ya ardhi ya nchi hiyo.

No comments: