Askari usalama wasiopungua 12 wa Kenya wameuawa na wengine kadhaa
kujeruhiwa baada ya wanamgambo wa al Shabab kuushambulia msafara wa
askari hao uliokuwa ukitoka katika mji wa Maua na kuelekea kwenye
Kaunti ya Mandera iliyoko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Noah
Mwivanda, Kamanda wa Polisi Kaunti ya Mandera amethibitisha taarifa za
kutokea shambulio hilo na kusema kwamba, maafisa wengine wanne wa KPR
wamejeruhiwa kwenye shambulio hilo na wanapatiwa matibabu kwenye
hospitali ya Mandera. Wakati huohuo,Serikali ya Kenya imetangaza
kuimarisha zaidi ulinzi na usalama karibu na majengo ya balozi za
kigeni, majengo ya jumuiya za kimataifa, majengo ya serikali na kwenye
miundombinu muhimu ya nchi hiyo ili kukabiliana na tishio la kutokea
mashambulio ya kigaidi katika mji mkuu wa nchi hiyo Nairobi. Polisi ya
Kenya imetangaza kuwa, ulinzi mkali umewekwa kwenye uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi na abiria wote wanaoingia
wanapaswa kukaguliwa kikamilifu. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya
kutolewa indhari ya tishio la mashambulizi ya kigaidi nchini humo.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, katika wiki za hivi karibuni Kenya imekuwa
ikishuhudia miripuko ya mara kwa mara inayofanyika hasa kwenye mabasi ya
abiria na kusababisha makumi ya watu kuuawa na kujeruhiwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment