Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Russia: Kiev iondoe wanajeshi mashariki Ukraine

Russia imeitaka serikali ya mpito ya Kiev kuondoa haraka vikosi vyake katika eneo la mashariki mwa Ukraine, huku ikiamuru kusitishwa maneva ya kijeshi yanayofanywa na wanajeshi wa Russia katika eneo linalopakana na Ukraine.  Taarifa iliyotolewa leo na ikulu ya Kremlin imeeleza kuwa, Rais Vladmiri Puttin wa Russia imetaka kuhitimishwa mara moja kile alichokiita kuwa ni maamuzi ya operesheni za adhabu dhidi ya wanaharakati wanaoungwa mkono na Moscow kwenye eneo la mashariki la Ukraine.

Hatua hiyo inaonekana kuwa ni jitihada zinazofanywa na Russia ili kupunguza mgogoro na nchi za Magharibi. Hata hivyo wanaharakati wanaoungwa mkono na Russia ambao wanadhibiti majengo ya serikali mashariki mwa Ukraine na kupigana na vikosi vya serikali ya Kiev wameapa kukwamisha uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika Jumapili, hasa katika maeneo yaliyotangaza kujitawala ya Donetsk na Luhansk.

No comments: