Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, May 21, 2014

Rais Rouhani: Silaha za mauaji ya umati ziangamizwe

Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa mara nyingine amesisitiza ulazima wa kushirikiana na kuunganisha nguvu kikamilifu katika kuangamiza silaha za mauaji ya kimbari ili kuimarisha amani na usalama duniani. Dakta Rouhani amesema hayo alipohutubia Mkutano wa CICA huko Shanghai China na kuongeza kuwa njia pekee ya kuondoa hatari ya silaha hizo ni kuziangamiza kikamilifu.
Rais wa Iran pia amezitaka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuimarisha nafasi ya nchi za Asia ili ziwe na taathira katika kuhakikisha kuwa dunia haina silaha za nyuklia.
Raouhani aidha amekumbusha kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutokana na sera zake za ulinzi na misingi ya kidini inapinga silaha za nyuklia lakini inaunga mkono haki ya nchi zote ya kutumia teknolojia ya atomiki kwa matumizi ya amani.

No comments: