Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

'Marekani haitoruhusiwa kukanyaga mstari mwekundu"

Kamanda wa ngazi za juu katika jeshi la Iran amesema taifa hili halitaruhusu Marekani kukanyaga mstari mwekundu katika mazungumzo ya nyuklia yanayoendelea kati ya Tehran na kundi la 5+1. Brigedia Jenerali Masoud Jazayeri amesema mafanikio ya kijeshi na kiulinzi ya Iran ni mstari mwekundu na kwamba Marekani isijaribu kuwashinikiza wanadiplomasia wa Tehran wakubali kulegeza kamba katika sekta hiyo. Afisa huyo mwandamizi wa jeshi la Iran amewataka wanadiplomasia wa Tehran kuwa macho dhidi ya njama hizo za Marekani na waitifaki wake kwenye kundi la 5+1.

Katika miezi ya hivi karibuni Marekani imekuwa ikisema kuwa, makubaliano ya mwisho ya Iran na kundi la 5+1 ambayo yatapelekea kuondolewa vikwazo vyote dhidi ya taifa hili sharti yajumuishe mambo mengine yasiyohusiana na kadhia ya nyuklia. Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na suala la haki za binadamu, wafungwa wa kisiasa, na uwezo wa kijeshi wa Iran. Washington inataka Tehran ipunguze kasi katika jitihada zake za kujiimarisha kijeshi na kiulinzi. Iran imesisitiza kuwa mazungumzo yanayoendelea ni ya nyuklia tu na wala hakuna suala lingine likatalojadiliwa nje ya kadhia ya nyuklia.

No comments: