Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Jamii ya kimataifa yalaani ghasia kaskazini mwa Mali

Jumuiya mbalimbali kama vile Umoja wa Afrika, Umoja wa Ulaya, ECOWAS pamoja na wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamelaani ghasia na machafuko ya hivi karibuni katika eneo la Kidal, kaskazini mwa Mali. Taarifa ya jumuiya hizo imesema mapigano yaliyoripotiwa hivi karibuni kati ya vikosi vya serikali ya Mali na wapiganaji wa makundi ya waasi ni ukiukaji wa makubaliano ya amani yaliyosainiwa na pande mbili hizo nchini Burkina Faso mwezi Machi mwaka uliopita. Jumuiya hizo zimesisitiza udharura wa kufanyika mazungumzo ya haraka kati ya pande hasimu ili hali ya utulivu irejee mara moja.

Siku ya Jumamosi kulitokea makabiliano makali kati ya waasi na jeshi la serikali katika eneo la Kidal ambapo watu kadhaa waliuawa na wengine kujeruhiwa. Mapigano hayo yalitokea wakati Waziri Mkuu wa Mali, Musi Mara alipokuwa ziarani katika eneo hilo la Kidal. Baadhi ya duru zinasema waasi wamewateka nyara watu 30 wakati wa patashika hiyo. Wapinzani wa serikali wanaojumuisha kundi la Tuareg na lile la Ansaru Din wanapigania kujitenga eneo la kskazini mwa Mali.

No comments: