Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 16, 2014

Lebanon yataka UN izuie uchokozi wa Israel

Afisa wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon anayeshughulikia masuala ya kigeni ameutaka Umoja wa Mataifa uchukue hatua za kukabiliana na chokochoko na mashambulio ya mara kwa mara ya Israel dhidi ya nchi hiyo. Amar Musawi amesema hayo katika mazungumzo yake na Derrick Plambly mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Lebanon na kusema kuwa, mashambulio na ukiukaji wa mara kwa mara wa mipaka ya ardhi ya Lebanon unaofanywa na Israel umekithiri na kwamba Umoja wa Mataifa unapaswa kuchukua hatua madhubuti na za kivitendo kuzuia suala hilo.

Afisa huyo wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon pia ameutaka Umoja wa Mataifa kuzingatia madhara ya mgogoro wa Syria na hasa kadhia ya wakimbizi wa nchi hiyo walioko Lebanon na jamii ya kimataifa kuisaidia serikali ya Beirut katika suala hilo.

No comments: