Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, May 22, 2014

HRW yasema Somalia inakiuka haki za wafungwa

Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeituhumu serikali ya Somalia kuwa inatumia vibaya mahakama za kijeshi kuwahukumu bila uadilifu mamia ya wafungwa huku ikiwanyima haki za kuwa na mawakili wa kuwatetea. 
Shirika hilo limesema kuwa mamia ya raia wa Somalia wameshitakiwa katika mahakama za kijeshi na kuhukumiwa bila kuzingatiwa sheria na viwango vya kimataifa. Shirika hilo la kutetea haki za binadamu pia limesema, raia wengi wamejikuta matatani baada ya kukamatwa katika msako wa kitaifa unaofanywa na mashirika ya kijasusi ya Somalia na wengi huwekwa vizuizini kwa muda mrefu bila kufunguliwa mashtaka.

Human Rights Watch imetoa ripoti iliyoashiria zaidi ya kesi 24 zilizosikilizwa na kuamuliwa kwa muda wa chini ya siku 4 na kusema kuwa serikali ya Somalia inapaswa kufanya mabadiliko na kuhamishia kesi za raia katika mahakama za kawaida.

No comments: