Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, May 22, 2014

Burundi yataka kustafidi na uwezo wa kielimu wa Iran

Omar Nazrin Ntezimbere, balozi wa Burundi hapa nchini amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imepiga hatua kubwa katika uwanja wa elimu na teknolojia na kusisitiza kwamba nchi zinazoendelea zinapaswa kustafidi na uwezo wa kielimu na kiteknolojia wa Iran. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea kituo cha utafiti wa nyuklia katika mkoa wa Alborz, Balozi Ntezimbere amesema kuwa, Iran  licha ya kupiga hatua kubwa kielimu ni nchi muhimu ulimwenguni kutokana na kuwa na ustaarabu na utamaduni mkongwe.
Balozi wa Burundi hapa mjini Tehran ameongeza kuwa, nchi ambazo zinataka kupiga hatua kimaendeleo zinaweza kushirikiana na Iran katika nyanja mbalimbali zikiwemo za elimu na teknolojia. Inafaa kuashiria hapa kuwa, viongozi wa ngazi za juu wa Iran mara kwa mara wamekuwa wakisisitiza juu ya kulipa kipaumbele  bara la Afrika katika sera zao za kigeni.
Katika upande mwingine Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA wamekubaliana juu ya hatua mpya tano zitakazochukuliwa ili kuimarisha zaidi mashirikiano ya pande mbili.

No comments: