Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, December 25, 2013

Idadi ya vifo katika mripuko Misri vyaongezeka

Idadi ya watu waliouawa katika mripuko uliotokea kwenye makao makuu ya polisi katika mji wa Mansoura huko Misri imeongezeka na kufikia 14. Bomu lililokuwa limetegwa ndani ya gari liliripuka mapema leo kwenye makao makuu ya polisi ya mji wa Mansoura ulioko umbali wa kilomita 110 kaskazini mwa Cairo katika wilaya ya Dakahlyia. Jengo zima limeporomoka na magari kadhaa yaliyokuwa nje ya makao makuu ya polisi yameharibika kutokana na mripuko huo mkubwa wa bomu uliotokea leo.
Watu 14 wamepoteza maisha katika mripuko huo huku wengine zaidi ya 100 wakijeruhiwa. Sami al Mihi Mkuu wa polisi wa wilaya ya Dakahlyia ni miongoni mwa watu waliojeruhiwa katika mripuko huo wa bomu huku washauri wake wawili wakiuawa.

No comments: