Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, July 14, 2013

Maelfu ya Wakongomani wamekimbilia Uganda

Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limetangaza kuwa, maelfu ya Wakongomani wamekimbilia katika nchi jirani ya Uganda kufuatia machafuko yanayoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.  Maafisa wa Umoja wa Mataifa wanasema kuwa, zaidi ya raia elfu thelathini wamekimbia makazi yao mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuingia nchini Uganda.
Taarifa zaidi zinasema kuwa, wakimbizi hao kwa sasa wamepatiwa hifadhi katika eneo la Bundibugyo magharibi mwa Uganda.
Wakati huo huo, hali katika jimbo la Kivu Kaskazini inaripotiwa kuanza kurejea katika hali ya kawaida baada ya jeshi kudhibiti jimbo hilo jana usiku. Katika upande mwingine, jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limefanikiwa kuyadhibiti maeneo ya mpaka wake na Uganda. Majeshi ya Congo yamewasili katika maeneo hayo na kufanikiwa kuwafurusha wapiganaji wa kundi la waasi la ADF-NALU linalopigana dhidi ya serikali ya Kampala.

No comments: