Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, July 12, 2013

Sudan yasisitiza kuheshimu makubaliano na S/Kusini

Serikali ya Sudan imesisitiza kuwa itaendelea kuheshimu makubaliano ya ushirikiano kati yake na Sudan Kusini. Hayo yamesemwa na Waziri wa Mafuta wa Sudan, Awad Ahmad al Jaz na kuongeza kuwa, Khartoum inalipa umuhimu mkubwa suala la kudumishwa usalama na amani kati ya nchi hizo mbili na kutekelezwa makubaliano yaliyofikiwa baina yao. Katika mazungumzo yake na na balozi wa Umoja wa Ulaya mjini Khartoum, Bwana al Jaz amesema kuwa, Sudan haijawahi kuwa na chaguo jingine ghairi ya kuimarisha usalama katika mipaka ya pamoja na Sudan Kusini na kwamba, hilo ni kwa manufaa ya nchi mbili katika ramani ya kutekeleza makubaliano ya pamoja.
Ameongeza kuwa, pamoja na Sudan Kusini kuvishambulia visima vya mafuta ambavyo ni mali ya Sudan huko katika eneo la Heglig mwezi Aprili mwaka jana, lakini serikali ya Khartoum ilikubali kusaini makubaliano ya ushirikiano na serikali ya Juba huku ikiendelea kusafirisha mafuta ya Sudan Kusini kupitia mabomba yake ndani ya ardhi ya Sudan. Kwa upande wake, balozi huyo wa Umoja wa Ulaya nchini Sudan alisisitiza kuwa, ushirikiano na mawasiliano baina ya Khartoum na Umoja wa Afrika kwa ajili ya kumaliza tofauti zilizopo kati ya nchi mbili, ni suala la lazima.

No comments: