Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Mashirika ya kijamii yaishtaki Marekani kwa ujasusi

Zaidi ya mashirika 19 ya kijamii nchini Marekani yamewasilisha kesi kortini yakiishtaki serikali ya nchi hiyo kwa kufanya ujasusi usio halali dhidi ya mabilioni ya watu kote duniani. Mashirika hayo yameitaka mahakama kuishurutisha serikali isimamishe mara moja ujasusi huo. Mawakili wa mashirika hayo ya kijamii nchini Marekani wamesema hatua ya serikali ya kudukua baruapepe za watu pamoja na akaunti zao kwenye mitandao ya kijamii,
kusikiliza mazungumzo ya simu kwa siri na kuweka vinasasauti katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kunasa mazungumzo ya wanadiplomasia ni kinyume na katiba ya Marekani na vilevile sheria za kimataifa. Majuma kadhaa yaliyopita, afisa wa zamani wa shirika la kijasusi la Marekani CIA Bw. Edward Snowden alifichua kwa mara ya kwanza mpango huo wa vyombo vya kijasusi vya Washington wa kuwafanyia ujasusi watu kote duniani. Ufichuzi huo umeiweka pabaya Marekani na kwa sasa Washington inamtafuta kwa udi na uvumba Bw. Snowden ili kumfungulia mashtaka ya kile inachosema ni kuhatarisha usalama wa taifa.

No comments: