Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 15, 2013

AU yataka kusakwa walioshambulia UNAMID

Umoja wa Afrika AU umeitaka Sudan kuchukua hatua za lazima za kuwatia mbaroni wale wote waliofanya mashambulizi dhidi ya wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika (UNAMID) huko Darfur magharibi mwa Sudan. Bi. Nkosazana Dlamini Zuma, Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika leo ametoa taarifa akilaani shambulizi la kuvizia lililofanywa na watu wenye silaha dhidi ya doria ya askari wa UNAMID huko Darfur magharibi mwa Sudan.
Bi Nkosazana ametaka kutiwa mbaroni na kuhukumiwa watenda jinai hiyo. Taarifa ya AU imesisitiza kuwa hakuna kitu chochote kinachohalalisha kuuliwa watu wanaojitolea kurejesha amani  huko Darfur. Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amesema shambulio hilo la kuvizia halitawavunja moyo walinda amani wao na wataendeleza jitihada zao za kurejesha amani ya kudumu huko Darfur. Watu waliokuwa na silaha wamefanya shambulizi la kuvizia dhidi ya wanajeshi wa kikosi cha kulinda amani cha UNAMID huko Darfur na kuwauwa wanajeshi saba wa Tanzania na kuwajeruhi wengine 17.

No comments: