Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, July 14, 2013

Mursi kuchunguzwa kuhusu jinai Misri

Ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma Misri imesema imepokea malalamiko ambapo rais aliyetimuliwa madarakani Mohammad Mursi anakabiliwa na tuhuma za ujasusi, kuchochea mauaji ya waandamanaji na kuharibu uchumi.
Katika taarifa, ofisi ya mwendesha mashtaka imesema inachunguza malalamiko hayo na kwamba inatayarisha faili la mashtaka dhidi ya Mursi na viongozi wandamizi wa Harakati ya Ikhwanul Muslimin.
Watuhumiwa hao wanatazamiwa kusailiwa katika siku zijazo. Mashtaka hayo yanakuja karibu wiki mbili baada ya jeshi kumuondoa madarakani Mursi kufuatia maandamano yaliyoambatana na umwagaji damu. Huku hayo yakijiri wafuasi wa Mursi bado wako kwenye mitaa ya Cairo mji mkuu wa nchi hiyo na wameapa kuendeleza maandamano hadi atakaporejeshwa madarakani. Kwingineko Waziri Mkuu wa Muda Misri Hazem el-Beblawi amesema wiki ijayo atatangaza baraza lake la mawaziri katika fremu ya 'ramani ya njia' inayoungwa mkono na jeshi ili kurejesha utawala mikononi mwa raia.

No comments: