Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, July 14, 2013

Mshukiwa wa mauaji ya Rwanda anaswa Ufaransa

Kanali wa zamani katika Jeshi la Rwanda ambaye alikuwa akisakwa kwa kuhusika katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini humo ametiwa mbaroni nchini Ufaransa.
Imearifiwa kuwa Kanali Laurent Serubuga alitiwa mbaroni Alkhamisi karibu na mji wa Cambrai kaskazini mwa Ufaransa. Wakili wake, Thierry Massis amesema Serubuga mwenye umri wa miaka 75 atafikishwa mahakamani Alkhamisi ijayo.
Imearifiwa kuwa katika mauaji ya kimbari ya Rwanda yaliyojiri kati ya Aprili na Julai mwaka 1994, Serubuga alikuwa naibu mkuu wa jeshi. Katika kipindi hicho watu zaidi ya laki nane waliuawa wakati watu wa Kabila la Hutu walipochochewa kutekeleza mauaji dhidi ya Watutsi.
Alain Gauthier mkuu wa kundi la waathirika wa mauaji ya kimbari Rwanda CPCR amesema kutiwa mbaroni Serubuga ni 'habari nzuri'. Ameongeza kuwa kanali Serubuga anapaswa kubeba lawama sawa na kanali Theoneste Bagosora. Itakumbukwa kuwa mwaka 2011 Mahakama ya Kimatiafa ya Jinai za Rwanda ilimtaja Bagosora kuwa mratibu mkuu wa mauaji ya kimbari ya Rwanda na kumhukumu kifungo cha miaka 35 gerezani. Serikali ya Rwanda kwa mara kadhaa imewatuhumu maafisa wa ngazi za juu wa Ufaransa kuwa walihusika katika mauaji hayo ya kimbari.

No comments: