Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Ustawi ya
Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), wanatarajiwa kukutana kuanzia kesho
hadi Julai 13 nchini Tanzania. Mawaziri hao wanatarajiwa kujadili
masuala mbalimbali ikiwemo hali ya kisiasa kusini mwa Afrika,
uimarishaji wa demokrasia, Utekelezaji wa Mpango na Mkakati wa Asasi ya
Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, mikataba ya ushirikiano katika nyanja
za Ulinzi na Usalama pamoja na ushirikiano baina ya SADC na Umoja wa
Ulaya (EU).
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa ya Tanzania, imesema kuwa, kikao hicho kitatanguliwa na
cha makatibu wakuu na maofisa waandamizi kitakachofanyika Julai 10 na 11
ambacho kitahudhuriwa na nchi zote wanachama wa SADC isipokuwa
Madagascar, ambayo imesimamishwa uanachama katika jumuiya hiyo. Taarifa
hiyo imebainisha kwamba, mawaziri hao watakutana Julai 13, chini ya
uenyekiti wa Bernard Membe Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment