Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 10, 2013

Utulivu watanda kwenye jengo la gadi ya rais Misri

Hatimaye usalama umerejea kwenye jengo la idara ya gadi ya rais nchini Misri. Hatua hiyo imekuja baada ya kupita siku moja ya umwagaji mkuwa wa damu, katika mapigano yaliyotokea mbele ya jengo hilo la gadi ya rais kati ya wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani Muhammad Mursi na jeshi la nchi hiyo na kusababisha zaidi ya watu 50 kuuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa. Usalama umetanda tangu asubuhi huku idadi ya askari wakipunguzwa eneo hilo.
Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov, ametangaza kuwa, nchi yake inaunga mkono hatua ya kurejeshwa usalama na amani nchini Misri. Lavrov ameyasema hayo hii leo na kuongeza kuwa, Moscow inaunga mkono juhudi zote za kumaliza machafuko nchini ya Miri na kufanyika uchaguzi huru na wa haki nchini humo. Tangu alipopinduliwa Rais Muhammad Mursi wa nchi hiyo, taifa hilo la kaskazini mwa Afrika limekuwa likishuhudia machafuko huku Umoja wa Afrika ukiwa tayari umesimamisha kwa muda uanachama wa Misri katika umoja huo. Mapema leo idara ya habari na mawasiliano ya ikulu ya rais nchini Tunisia, imekanusha kuhusika kivyovyote na suala la kusimamishwa uanachama wa Cairo katika Umoja wa Afrika. Itakumbukwa kuwa, Tunisia ni miongoni mwa nchi zilizopinga mapinduzi ya jeshi la Misri dhidi ya Rais Mursi na kuitaja kuwa ni ukandamizaji wa demokrasia.

No comments: