Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 10, 2013

UNICEF yalaani shambulio dhidi ya shule Nigeria

Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF umelaani shambulio la kundi la Boko Haram dhidi ya shule moja ya bweni nchini Nigeria. Taarifa ya UNICEF imebainisha kwamba, shambulio hilo lililosababisha wanafunzi 28 na mwalimu mmoja kuuawa kinyama baada ya shule yao kuchomwa moto ni jinai ya wazi hivyo waliotenda jinai ni lazima wafuatiliwe kisheria.

Aidha jana Umoja wa Ulaya nao ulilaani vikali mauaji ya kikatili dhidi ya wanafunzi wa shule hiyo ya sekondari ya bweni nchini Nigeria. Bi Catherine Ashton, Mkuu wa Siasa za Nje za Umoja wa Ulaya sambamba na kulaani mauaji hayo alitaka magaidi waliofanya jinai hiyo kufuatiliwa kisheria.  Viongozi wa Nigeria wametangaza kwamba, waliohusika na jinai hiyo watafikiwa na mkono wa sheria.
Wakati huo huo, viongozi wa Nigeria wametangaza kufungwa shule za sekondari katika jimbo la Yobe kufuatia mauaji ya wanafunzi wa shule ya msingi yaliyofanywa siku ya Jumamosi.

No comments: