Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 10, 2013

Nigeria, Boko Haram waafiki kusimamisa mapigano

Serikali ya Nigeria na kundi la Boko Haram, wamekubaliana kusimamisha mapigano ya pande mbili. Makubaliano hayo yamekuja kwa mnasaba wa kuwadia mwezi mtukufu wa Ramadhani. Mkuu wa tume ya kufanya mazungumzo na Boko Haram, Bwana Tanimu Turaki amewambia waandishi wa habari kuwa, makubaliano hayo ya usitishaji mapigano kati ya serikali na kundi hilo, yamefikiwa baada ya mazungumzo ya muda mrefu kati ya pande hizo mbili.
Tume hiyo imeundwa na Rais Goodluck Jonathan wa nchi hiyo, kwa lengo hilo. Aidha tume hiyo yenye wajumbe 26, inafanya juhudi za kuwapokonya silaha wanamgambo wa kundi hilo. Turaki ameongeza kuwa, mazungumzo hayo kati ya serikali na kundi la Boko Haram, yamewashirikisha wanachama 104 wa kundi hilo na yamefanyika katika moja ya magereza ya mjini Lagos. Hii ni katika hali ambayo gavana wa jimbo la Yobe la kaskazini mwa Nigeria ameamuru kufungwa shule zote za sekondari katika jimbo hilo hadi mwezi Septemba baada ya kutokea maafa ya kuuawa watu 42 katika shule moja jimboni humo. Wanafunzi 41 wa shule hiyo ya sekondari na mwalimu wao mmoja waliuawa katika shambulizi lililofanywa na watu waliokuwa na silaha na wanaosadikiwa kuwa ni wanamgambo wa Boko Haram katika mji wa Mamudo, jimboni humo.

No comments: