Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 15, 2013

Al Baradei aapishwa Ikhwan waitisha maandamano

Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia IAEA amekula kiapo cha kuchukua wadhifa wa Makamu wa Rais nchini Misri. Muhammad al Baradei amekula kiapo hicho mbele ya Adly Mansour, Rais wa serikali ya Mpito ya Misri.
Wakati huo huo harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri na mirengo mingine ya Kiislamu ya nchi hiyo imetoa wito wa kufanyika maandamano ya mamilioni ya watu dhidi ya serikali ya Adly Mansour, Rais wa serikali ya mpito ya nchi hiyo.

Wanaharakati wa Misri wametangaza kuwa maandamano hayo yatafanywa kesho na wafuasi wa Morsi katika meidani za Rabaa Adawiya, Nahdha, al Jizah, Ramsis na kwenye daraja la Oktoba Sita.
Hii ni katika hali ambayo wapinzani wa Muhammad Morsi, rais wa Misri aliyeng'olewa madarakani na jeshi la nchi hiyo nao pia wamejiandaa kikamilifu kufunga barabara zinazoelekea kwenye meidani hizo khususan kwenye daraja la Oktoba Sita, meidani ya Lebanon na kitongoji cha Nasr na njia ya chini kwa chini ya Nasr.

No comments: