Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, July 4, 2013

Mursi: Niko tayari kufa kwa ajili ya demokrasia

Rais Mohammad Mursi wa Misri ameapa kwamba hatoondoka madarakani na kwamba yuko tayari kufa kwa ajili ya kutetea demokrasia. Akizungumza usiku wa jana kupitia radio na televisheni ya taifa, kiongozi huyo aliwaambia wapinzani wake kuwa, alichaguliwa kihalali na kwamba ataendelea na majukumu yake hadi kipindi chake kitakapomalizika. Wafuasi wake pia wameapa kumlinda kiongozi huyo na kwamba wako tayari kufa kwa ajili yake. Wapinzani kwa upande wao wamesisitiza kuwa maandamano yataendelea hadi pale Dkt. Mursi atakapojiuzulu.
Weledi wa mambo wanasema Misri inaelekea kutumbukia katika vita vya ndani hususan baada ya jeshi kusema huenda likachukua jukumu la kuiongoza nchi iwapo pande hasimu hazitofikia makubaliano kufikia leo jioni.

No comments: