Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Ujumbe wa kidiplomasia wa Ethiopia wawasili Cairo

Ujumbe wa kidiplomasia wa Ethiopia ukiongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na mkuu wa kituo cha amani wa nchi hiyo, wamewasili mjini Cairo, Misri kwa ajili ya kushiriki katika kikao cha siku tatu mjini humo. Hii ni mara ya kwanza kwa ujumbe wa kidiplomasia wa Ethiopia kufanya safari nchini Misri tangu serikali ya Addis Ababa ilipotangaza kujenga bwawa la an-Nahdha na kuibuka mzozo kati ya nchi mbili. Weledi wa kimataifa wanaamini kuwa, ujenzi wa bwawa hilo katika mto Nile, hauwezi kuathiri maslahi ya nchi za Sudan na Misri.
Weledi hao wa kimataifa kutoka nchi za Ethiopia, Sudan, Misri, Ufaransa, Ujerumani, Afrika Kusini na Uingereza, wameanza kufanya uchunguzi wa athari zinazoweza kutokea kutokana na kujengwa bwawa hilo. Hivi karibuni Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Desalegn alitia saini mkataba wa ugawanaji sawa wa maji ya Mto Nile miongoni mwa nchi unakopita mto huo. Hii ni katika hali ambayo, Rais Yoweri Museven wa Uganda ametangaza kuiunga mkono serikali ya Addis Ababa juu ya kujenga bwawa hilo kwa ajili ya kuzalisha umeme. Kwa upande wake gazeti la The Wall Street Journal limeripoti kuwa, Ethiopia na nchi nyingine za Afrika zenye kutumia mto Nile, zinahitaji kujenga mabwawa kwa ajili ya kujizalishia umeme wao.

No comments: