Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Watoto wa Mubarak waendelea kushikiliwa

Idara inayofuatilia mapato na utajiri wa raia wa Misri kinyume cha sheria ambayo ni kitengo katika Wizara ya Sheria ya nchi hiyo,  imeongeza muda wa siku 15 za kuendelea kuwashikilia wana wa dikteta wa zamani Hosni Mubarak kwa ajili ya kuwafanyia mahojiano zaidi. Habari kutoka Cairo zinaarifu kuwa Alaa na Jamal wakiwa na ulinzi mkubwa, walifikishwa katika idara hiyo ya Wizara ya Sheria kwa tuhuma za kutumia vibaya madaraka ya baba yao wakati akiwa rais wa nchi hiyo na kujikusanyia utajiri mkubwa, kumiliki hisa nyingi katika benki na kumiliki mali nyingine nyingi kinyume cha sheria.
Kikao cha mahakama kwa ajili ya kuchunguza faili la wana hao wa dikteta Mubarak, kinatazamiwa kufanyika leo Jumatatu. Hii ni katika hali ambayo tangu mwezi Mei mwaka 2011 idara hiyo inayochunguza mapato ya raia wa nchi hiyo, imekwishawahoji Alaa na Jamal kwa tuhuma hizo huku kukiwa hakujachukuliwa hatua yoyote dhidi yao. Hivi karibuni pia Mahmud al-Hafnawi, mwakilishi wa mwendesha mashtaka mkuu nchini Misri aliutaja utajiri wa Mubarak na familia yake kuwa unafikia karibu dola bilioni moja na milioni 200.

No comments: