Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 14, 2013

Porojo dhidi ya Syria zaendelea, US kuwaauni magaidi

Katika kile kinachoonekana ni kuendelea propaganda dhidi ya serikali halali ya Syria, Umoja wa Mataifa umetoa ripoti inayosema hadi sasa zaidi ya watu 93, 000 wameuawa kwenye machafuko nchini humo. ripoti hiyo imekwenda mbali na kusema maafa mengi yamesababishwa na serikali ya Rais Bashar Asad. Huku hayo yakijiri, Marekani imezusha propaganda mpya na kusema sasa upo ushahidi kamili kwamba, serikali ya Syria ilitumia silaha za kemikali dhidi ya raia.
Rais Barack Obama wa Marekani ameidhinisha kupewa silaha magaidi wa Syria wanaopigana na serikali akisema Asad amekanyaga msitari mwekundu. Taarifa kutoka ikulu ya White House imesema Marekani itatoa misaada ya moja kwa moja ya kijeshi kwa makundi ya waasi huko Syria na kwamba misaada hiyo itajumuisha silaha nzito.

No comments: