Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 14, 2013

Watu 93,000 wameuawa katika mgogoro wa Syria

Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, watu wasiopungua 93,000 wameuawa nchini Syria katika mapigano ya wanamgambo wanaofadhiliwa na nchi za kigeni dhidi ya serikali ya Rais Bashar al Assad kwa zaidi ya miaka miwili sasa.  Navi Pillay Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, tangu Julai mwaka uliopita watu 5,000 wamekuwa wakiuawa kila mwezi kwenye mapigano hayo.
Pillay ameongeza kuwa, takwimu hizo ni za kipindi cha kati ya Machi mwaka 2011 hadi mwishoni mwa Aprili 2013 na kwamba kati ya wahanga hao wa vita nchini Syria, 6,561 ni vijana wadogo na zaidi ya 1,729 ni watoto walio na umri chini ya miaka 10.
Katika upande mwingine Marekani imesema kuwa inaongeza msaada wa kijeshi kwa waasi wa Syria wanaopigana dhidi ya serikali, kwa madai kuwa Damascus eti imetumia silaha za kemikali kwenye mapigano hayo dhidi ya waasi.

No comments: