Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 27, 2013

Kissinger: Vyombo vya habari Marekani vinapotosha

Waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani Henry Kissinger amesema kuwa vyombo vya habari vya nchi hiyo vinasema urongo kuhusu hali ya mambo nchini Syria.
Kissinger ambaye alikuwa akihutubia katika Chuo Kikuu cha Michigan amesema, vyombo vya habari vya Marekani vinapotosha ukweli wa mambo na havisemi ukweli kuhusu habari zinazohusiana na Syria.

Amesema kuwa vyombo hivyo vinamtambulisha Rais Bashar Assad wa Syria kuwa ni dikteta anayeua wananchi wake na kwamba waasi ni wanademokrasia. Waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani amesema upotoshaji huo unafanyika katika fremu ya siasa makhsusi.
Matamshi hayo ya Kissinger yametolewa wakati Marekani inakosolewa kwa kuchochea fitina za kimadhehebu nchini Syria na katika nchi nyingine za Mashariki ya Kati kwa kuingilia mambo ya ndani ya nchi hizo.

No comments: