Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 27, 2013

UN: Uwekezaji wa kigeni Afrika umeongezeka

Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa nchi za Afrika zimeshuhudia ongezeko la uwekezaji wa kigeni katika mwaka uliopita wa 2012.
Umoja wa Mataifa umesema uwekezaji wa kigeni katika nchi za Afrika uliongezeka kwa dola bilioni 50 katika mwaka 2012. Taarifa ya UN imesema kuwa, nchi za Afrika ni miongoni mwa nchi ambazo zina ustawi mkubwa zaidi wa uchumi duniani.

Ripoti hiyo inasema kuwa ustawi wa uchumi wa nchi za Afrika umepatikana katika hali ambayo uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni katika nchi mbalimbali za dunia katika mwaka 2012 umepungua kwa asilimia 18.
Aprili mwaka huu pia Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) ulitangaza kuwa uchumi wa nchi za Kiafrika unaendelea kustawi vizuri.

No comments: