Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 27, 2013

Wapinzani Guinea wataka kudhaminiwa usalama

Kambi ya upinzani nchini Guinea Conakry imetangaza kuwa haitafanya mazungumzo ya aina yoyote ya wawakilishi wa serikali ya nchi hiyo ila baada ya kudhaminiwa usalama wa viongozi wake.
Viongozi wa kambi ya upinzani nchini Guinea wamesema kuwa sharti la kufanya mazungumzo na serikali ya Conakry ni kudhaminiwa usalama kamili wa viongozi wa upinzani.
Msemaji wa muungano wa kambi ya upinzani Abu Bakr Silla amesema viongozi wa kambi hiyo wameamua kusitisha mazungumzo ya kitaifa hadi pale watakapopewa madhamana ya usalama wao na kuondolewa vizingiti vyote vinavyowakabili.

Amekosoa ukandamizaji unaofanywa na serikali dhidi ya wanaharakati wa vyama vya upinzani na kusisitiza kuwa ni ukiukaji wa sheria za nchi.

No comments: