Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

Iran yakanusha madai ya Canada kuhusu uchaguzi

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Abbas Araqchi, amepuuzilia mbali matamshi ya hivi karibuni ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, John Baird, kuhusu uchaguzi wa rais uliofanyika Juni 14 katika Jamhuri ya Kiislamu. Katika matamshi yake hivi karibuni, Baird ambaye ana tabia ya kutoa matamshi ya kijeuri ya kuuingilia mambo yasiyomuhusu, alidai kuwa, uchaguzi wa Rais Iran eti haukuwa na maana.
Msemaji wa Wizara Mambo ya Nje ya Iran alipoulizwa kuhusu matamshi hayo ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada amesema, haoni haja hata ya kujibu matamshi hayo. Amesema waziri huyo wa Canada ana tabia ya kutoa matamshi kama hayo jambo ambalo linatilia shaka uwezo wake wa kutathmini masuala ya kisiasa. Kuhusu machafuko yanayoendelea hivi sasa nchini Uturuki, Araqchi ametoa mwito kwa wananchi wa Uturuki na serikali ya nchi hiyo kujizuia kueneza mgogoro uliopo. Amekanusha madai kuwa Iran inaingilia masuala ya ndani ya Uturuki na kusema, Waziri Mkuu wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan anapaswa kutii matakwa ya wananchi. Akijibu swali kuhusu iwapo sera za kigeni za Iran zitabadilika baada ya kuchaguliwa Sheikh Hassan Rohani kama  rais, Araqchi amesema, sera za kigeni za Jamhuri ya Kiislamu zina msingi unaotegemea thamani na maslahi ya kitaifa na miongozo ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, na hivyo mkondo utaendelea kuwa huo isipokuwa mbinu za utekelezaji ndizo zinazoweza kubadilika.

No comments: