Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

China yajitahidi kumaliza hitilafu za Khartoum na Juba

China imesema kuwa, itafanya kila linalowezekana ili kuzisaidia Sudan na Sudan Kusini kufikia mapatano na hivyo kumaliza suutafahumu na hitilafu kati ya pande mbili hizo.
China imesema hayo leo kufuatia hatua ya hivi karibuni ya Sudan ya kukataa kusafirisha mafuta ya Sudan Kusini kupitia mabomba yake.
Ali Karti, Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan juzi alimueleza Zhong Jianhua, Mjumbe wa China barani Afrika kwamba, Sudan imeanzisha jitihada zote ili kufikia uhusiano wema na jirani yake Sudan Kusini.

Mjumbe wa China barani Afrika amesema kuwa, nchi yake itafanya kila linalowezekana ili kuziwezesha Khartoum na Juba kufikia mapatano na kutatua masuala yaliyosalia baina yao.

No comments: