Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 20, 2013

Afghanistan yasimamisha mazungumzo na Marekani

Msemaji wa Rais Hamid Karzai wa Afghanistan amesema kuwa, nchi hiyo imesimamisha mazungumzo na Marekani kuhusiana na makubaliano ya pande mbili ya kiusalama (BSA) kutokana na misimamo ya Washington. Amal Faizi amesema kuwa, kuna tofauti kati ya kile kinachosemwa na serikali ya Marekani na hatua inazochukua kuhusiana na mazungumzo ya amani ya Afghanistan.

Hayo yamejiri baada ya kuripotiwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya maafisa wa Marekani na wanamgambo wa kundi la Taliban. Pia Rais wa Afghanistan amekosoa kitendo cha kupewa Taliban ofisi ya kisiasa katika mji mkuu wa Qatar, Doha. Suala hilo pia limepingwa na wabunge wa Afghanistan. Karzai amesema serikali yake haitoshiriki mazungumzo yoyote na Marekani pamoja na kundi la Taliban hadi pale mazungumzo hayo yatakapoongozwa na serikali ya Kabul.

No comments: