Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 20, 2013

Obama ataka silaha za nyuklia zipunguzwe

Rais Barack Obama wa Marekani ametoa wito wa kufanywa jitihada za kupunguza silaha za nyuklia za nchi yake pamoja na Russia.
Akizungumza huko Brandenburg Gate katika safari yake kwenye mji mkuu wa Ujerumani, Berlin, Obama amesema kuwa ana uhakika Marekani inaweza kulinda usalama wake hata kama itapunguza silaha zake za nyuklia hadi theluthi moja na kuitaka Russia pia kufanya hivyo hivyo.

Matamshi hayo ya Obama yamejibiwa haraka na Naibu Waziri Mkuu wa Russia Dmitry Rogozin aliyesema kwamba, wito huo wa Obama wa kupunguza silaha za nyuklia hauwezi kuzingatiwa. Ameongeza kuwa, hatua ya Marekani ya kupelekea mitambo ya kuzuia makombora barani Ulaya ni kikwazo kikubwa cha kupunguza silaha za nyuklia kwa Russia.
Kremlin imesema kwamba, suala la kupunguzwa hifadhi kubwa ya silaha za nyuklia, halipaswi kuishia tu kwa nchi hizo mbili, bali linapaswa kujumuisha serikali nyingine zinazohodhi silaha hizo hatari.

No comments: