Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, February 3, 2013

Ufaransa yahalalisha ndoa za wanaolawitiana

Licha ya maandamano makubwa ya wananchi wa Ufaransa ya kupinga kuhalalishwa kisheria ndoa za watu wanaolawitiana, bunge la taifa la nchi hiyo limepasisha mswada wa sheria hiyo kwa wingi mkubwa wa kura.
Bunge la Ufaransa limepasisha kwa kura 249 za 'ndiyo' dhidi ya 97 za 'hapana' mswada wa sheria inayowaruhusu kuoana kisheria wanaume wanaolawitiana. Kama ilivyokuwa imetarajiwa, wabunge wa chama cha kisoshalisti, chama cha kijani na cha mrengo wa kushoto waliunga mkono mswada huo uliopingwa na wawakilishi wa chama cha umoja kwa ajili ya harakati ya wananchi. Wabunge wa mrengo wa kulia wameeleza wasiwasi walionao kutokana na kupasishwa mswada huo. Kupasisha sheria ya kuruhusu ndoa za watu wanaolawitiana ni moja ya ahadi zilizotolewa na Rais Francois Hollande wa Ufaransa wakati wa kampeni za uchaguzi kwa madhumuni ya kuvutia kura za makundi ya watu wa jinsia moja wenye mwenendo potofu wa maingiliano ya kimwili…/

No comments: