Hatua ya Rais Barack Obama wa Marekani kuonekana akifanya mazoezi
ya kulenga shabaha kwa bunduki, imetajwa zaidi na weledi wa masuala ya
kisiasa kuwa ni inayounga mkono vitendo vya matumizi ya silaha nchini
humo.
Picha hizo zilisambazwa na Ikulu ya White House na kuwatia wasi
wasi mkubwa wanaharakati wanaoitaka serikali ya Washington kupitisha
muswada wa sheria utakaopiga marufuku matumizi ya silaha kwa raia.
Kufuatia mauaji hivi karibuni katika shule ya msingi katika wilaya ya
New Town katika jimbo la Connecticut, Rais Barack Obama wa Marekani
aliahidi kuchukua hatua madhubuti kwa ajili ya kupunguza vitendo vya
kikatili vinavyotokana na matumizi ya silaha za moto. Hata hivyo kauli
hiyo ilikabiliwa na radiamali hasi kutoka kwa lobi ya waungaji mkono wa
matumizi hayo ya bunduki nchini humo. Weledi wanaamini kuwa, hatua ya
rais huyo kuonekana akifanya mazoezi ya kulenga shabaha kwa bunduki
inakinzana na kauli yake ya kupunguza vitendo vya kikatili nchini
Marekani.Sunday, February 3, 2013
Obama aonekana akitumia bunduki
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment