Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, February 3, 2013

Hollande: Vita nchini Mali havijamalizika

Rais wa Ufaransa Francois Hollande ambaye vikosi vya nchi yake vimevamia Mali kwa kisingizio cha kupambana na waasi, amesema kuwa, vita vya Ufaransa nchini humo havijamalizika. Rais  Hollande aliyasema hayo jana katika medani ya Uhuru mjini Bamako, mji mkuu wa Mali. Ameongeza kuwa, kadhia ya kushambulia Mali ilifikiwa mnamo tarehe 10 mwezi jana na kwamba, askari wa nchi yake wataendelea kubakia Mali kupambana na waasi. Hollande amedai kuwa, Ufaransa imeishambulia Mali kwa ushirikiano na jamii ya kimataifa chini ya uungaji mkono wa nchi za Ulaya.
Akiwa mjini Timbuktu kaskazini mwa Mali, rais huyo wa Ufaransa alisema kuwa, vikosi vya nchi hiyo vitaendelea na operesheni zake Mali na kwamba  vitakabidhi kwa awamu hatamu za uendeshaji operesheni hizo vikosi vya askari wapatao 8,000 wa nchi za Afrika. Nchi zinazounga mkono vita vya Ufaransa nchini Mali ni pamoja na Marekani, Canada, Uingereza, Ubelgiji, Ujerumani na Denmark. Weledi wa mambo wanasema lengo la vita vya Mali ni kupora utajiri mkubwa wa mali asili nchini humo kama vile mafuta, dhahabu na madini ya urani.

No comments: