Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, January 26, 2013

Viongozi wa AU kujadili migogoro ya Afrika

Wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika watajadili migogoro na vita vinavyoendelea kujiri nchini Mali, hitilafu baina ya Sudan na Sudan Kusini, mapigano ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Guinea Bissau na Jamhuri ya Afrika ya Kati kwenye kikao kitakachoanza kesho huko Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia. Tarifa zinasema kuwa, mapigano ya Mali na mpango wa kutumwa kikosi cha Umoja wa Afrika kwa shabaha ya kupambana na makundi yenye misimamo ya kufurutu mipaka kaskazini mwa nchi hiyo, ni miongoni mwa ajenda kuu za kikao cha wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika.
Hali kadhalika kikao hicho ambacho kitahudhuriwa pia na Ban Ki moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, kinatarajiwa kumpa uwenyekiti wa mzuguko wa Umoja wa Afrika Haile Mariam Desalegne Waziri Mkuu wa Ethiopia kutoka kwa Rais Thomas Yayi Boni wa Benin. Kikao cha wakuu wa wanachama wa Umoja wa Afrika kitaanza kesho Jumapili na kuendelea hadi Jumatatu nchini Ethiopia.

No comments: