Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, January 26, 2013

Turki Feisal ataka waasi wa Syria wapewe silaha

Turki al Feisal Mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Saudi Arabia ametaka makundi ya kigaidi nchini Syria yapewe silaha zaidi za kisasa ili yakabiliane vilivyo  na majeshi ya nchi hiyo. Al Feisal amekiri kwamba waasi hawana uwezo wa kukabiliana na jeshi la Syria na kuongeza kuwa makundi ya waasi yanayopambana na majeshi ya Syria lazima yapewe silaha na zana za kisasa za kivita zikiwemo za kutungulia ndege na vifaru. Turki al Feisal amepinga vikali kutumiwa njia za kidiplomasia za kuutatua mgogoro wa Syria na kuongeza kuwa, kuna udhaura wa kupewa waasi silaha za kisasa za kukabiliana na majeshi ya Syria.
Hivi karibuni, Walid Muallim Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Syria amesisitiza juu ya kukomeshwa usaidizi wa kifedha na kisilaha kwa makundi ya kigaidi nchini humo kwa lengo la kutatuliwa mgogoro wa Syria na kuongeza kuwa nchi za Qatar, Uturuki na Saudi Arabia zikiongozwa na Marekani zimekuwa zikitoa uungaji mkono mkubwa wa kifedha na kisilaha kwa makundi ya waasi na kigaidi nchini Syria.

No comments: