Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, January 26, 2013

36 wafariki dunia kwenye mafuriko nchini Msumbiji

Watu wasiopungua 36 wamefariki dunia na wengine wapatao elfu sabini wamekosa makaazi baada ya kunyesha mvua kubwa iliyosababisha kutokea mafuriko nchini Msumbiji. Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini Msumbiji imeeleza kuwa, watu 26 wamepoteza maisha katika eneo la kusini mwa jimbo la Gaza pekee. Mafuriko hayo yanatokana na mvua kubwa zilizonyesha katika nchi za Afrika Kusini na Zimbabwe na kusababisha kufurika maji katika Mto Limpopo. Nchi Afrika Kusini nako wiki iliyopita watu 12 walipoteza maisha baada ya kutokea mafuriko nchini humo. Brigedia Jenerali Xolani Mabanga wa jeshi la Afrika Kusini amesema kuwa, nchi hiyo imetuma helkopta mbili za kijeshi na kikosi cha waokoaji kwa lengo la kuwasidia wananchi wa Msumbiji waliokumbwa na maafa hayo. Aidha Afrika Kusini  imetuma ndege ya kijeshi ikiwa na timu za madaktari, wauguzi na wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu kwa lengo la kuwasaidia wananchi wa Msumbiji.

No comments: