Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, January 22, 2013

Viongozi mashuhuri wa kisiasa wa Madagascar wajiondoa katika uchaguzi ujao

Andry Rajoelina na Marc Ravalomanana wanasiasa mashuhuri na ambao pia ni marais wa sasa na zamani wa Madagascar kwa utaratibu wamejiondoa katika kinyang'anyiro cha kuwania urais wa baadaye wa nchi hiyo iliyoko katika bahari ya Hindi. Vita vya kuwania madaraka kati ya viongozi wawili hao vilianza mwezi Machi miaka minne iliyopita na hivyo kuvuruga utulivu wa kisiasa wa nchi hiyo. Maandamano makubwa yaliyoongozwa na Rajoelina ambaye wakati huo alikuwa meya wa mji mkuu Antananarivo yalimpelekea kujiuzulu Rais Marc Ravalomanana. Hata hivyo kabla ya kuondoka madarakani Ravalomanana aliwaachia madaraka majenerali wa jeshi ambao nao walimkabidhi madaraka hayo Rajoelina ambaye alikuwa kiongozi wa Baraza Kuu la Mpito. Umoja wa Afrika  na vyama vya upinzani vililichukulia tukio hilo kuwa ukiukaji wa wazi wa katiba ya nchi.
Kufuatia uingiliaji kati wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC, hatimaye mwezi Agosti mwaka uliopita vyama hivyo vilikubali kugawana madaraka na Rajoelina kwa kukubali kushiriki katika serikali ya mpito hadi wakati wa kufanyika uchaguzi mkuu mpya. Kufuatia mapatano hayo Rajoelina aliyeongoza mapinduzi ya Machi 2009 aliteuliwa kuwa rais wa serikali ya mpito. Licha ya hayo uchaguzi mkuu uliokuwa umepangwa kufanyika mwaka 2011 na 2012 uliakhirishwa kutokana na tofauti zilizojitokeza kati ya pande hasimu. Moja ya tofauti hizo zilitokana na mjadala mkali kuhusiana na uwezekano wa kurejea au kutorejea Marc Ravalomanana kutoka uhamishoni nchini Afrika Kusini. Ravalomanana alihukumiwa kifo bila ya kuwepo mahakamani na mahakama moja ya mjini Antananarivo kwa kosa la kuwaua waandamanaji walioshiriki maandamano ya kutaka kuiangusha serikali yake. Licha ya kutolewa msamaha wa wote nchini lakini hukumu ya mahakama hiyo ilimzuia Ravalomanana kujumuishwa kwenye msamaha huo. Pamoja na hayo lakini SADC iliingilia kati na kuvishawishi vyama vya kisiasa kukubali kurejea nchini Ravalomanana bila masharti yoyote. Kwa msingi huo mpango wa mwaka 2011 uliokuwa umekusudiwa kuleta maridhiano na umoja wa kitaifa kati ya pande hasimu za Madagascar haukutekelezwa.
Kwa kuzingatia kwamba sasa mahasimu hao wakuu wa kisiasa wamekubali kutoshiriki katika uchaguzi ujao wa rais wa Madagascar, kuna matumaini ya kurejea tena amani na utulivu nchini humo.

No comments: