Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, December 18, 2013

Wanamgambo wa Seleka wapokonywa silaha CAR

Zaidi ya wanamgambo 7000 wa kundi la Muungano wa Seleka, waasi wa zamani katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, wameamua kuweka chini silaha zao.
Hayo yamesemwa leo na mmoja wa makamanda wa ngazi za juu wa kikosi cha Afrika cha kulinda amani nchini humo MISCA. Ameongeza kuwa, wanamgambo wa Seleka wameanza kupewa hifadhi kwenye kambi na kiasi kidogo tu ndio wako nje ya kambi.
Kiongozi huyo ambaye hakutaka kutaja jina lake amesema kuwa, vikosi vya majeshi ya Kiafrika viko nchini humo kwa shabaha ya kurejesha amani na utulivu Bangui, mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, ambapo zaidi ya watu 600 wameuawa katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.
Nalo Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) limetangaza kuwa, karibu watu laki mbili na elfu kumi wameyakimbia makazi yao baada ya kushadidi machafuko mjini Bangui.

No comments: