Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, January 29, 2013

Mkutano wa viongozi wa AU wamalizika Ethiopia

Mkutano wa 20 wa wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika ulimalizika jana usiku huko Addis Ababa, Ethiopia makao makuu ya umoja huo.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Haile Mariam Desalegn ambaye pia ni Mwenyekiti wa umoja huo amesema kwenye hotuba yake ya kufunga mkutano huo kwamba, ulijadili kwa kina suala la amani na usalama, mapigano yanayoendelea katika baadhi ya nchi wanachama kama Mali, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo pamoja na mgogoro wa kisiasa wa Madagascar.

Desalegn ameongeza kuwa, wakuu wa AU wametangaza mshikamano  wao kwa serikali ya Mali na wamesisitiza juu ya kufanyika juhudi maradufu za kuiunga mkono serikali ya Bamako. Amesema, Umoja wa Afrika umeafiki kutoa msaada wa dola milioni hamsini kuvisaidia vikosi vya ulinzi na  usalama vya Mali. Mkutano wa 20 wa wakuu wa Umoja wa Afrika ulianza tarehe 27 hadi 28 ya mwezi Januari na umehudhuriwa na marais na viongozi wa ngazi za juu wa nchi 54 za umoja huo, wawakilishi wa taasisi za kimataifa na nchi wanachama watazamaji ikiwemo Iran.

No comments: