Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, January 29, 2013

Madaktari Bahrain wanateswa kwa kuwatibu majeruhi

Madaktari wa Bahrain wanakabiliwa na mateso makali wakiwa jela na korokoroni kwa kosa la kuwatibu wapinzani wa serikali ya nchi hiyo.
Daktari Nada Dhwayf amesema kuwa, katika kipindi alichowekwa mahabusu alikabiliwa na mateso makubwa kutoka vikosi vya usalama vya utawala wa Aal Khalifa wa nchi hiyo kwa kosa la kuwapa matibabu wanamapambano wa nchi hiyo. Daktari Dhwayf ameongeza kuwa, familia ya Aal Khalifa ndio inayopaswa kubebeshwa lawama za ukatili unaofanywa dhidi ya madaktari na wauguzi nchini humo.
Tokea kuanza kwa vuguvugu la mageuzi nchini Bahrain mwezi Februari mwaka 2011, karibu madaktari elfu mbili wameshatiwa mbaroni na suala hilo limesababisha wananchi wengi kupoteza maisha yao kwa kukosa huduma za tiba.

No comments: