Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, January 29, 2013

Jihadul Islami yakosoa matamshi ya Abbas

Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina imelaani vikali matamshi yaliyotolewa na Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina kuhusiana na mpango wa kuundwa serikali mbili za Palestina.
Khadhwar Habib mmoja kati ya viongozi waandamizi wa Jihadul Islami ya Palestina amesema kuwa, matamshi ya Mahmoud Abbas ya kutaka kuundwa serikali mbili za Palestina yanakinzana na malengo ya muqawama na mapambano ya wananchi wa Palestina dhidi ya Wazayuni, kwani mapambano ndiyo njia pekee itakayoweza kuzikomboa ardhi  za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa ghasibu wa Israel.
Habib amekosoa vikali msimamo wa Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina na kuongeza kuwa, ardhi ya kihistoria ya Palestina imeshikamana na kamwe wananchi wa Palestina hawako tayari kuutambua rasmi utawala wa Kizayuni wa Israel.

No comments: