Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, January 28, 2013

Iran kutuma misaada kwa wakimbizi wa Syria

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya nchi za Kiarabu na Kiafrika amesema kuwa, Tehran ipo tayari kutuma misaada ya kibinadamu kwa wakimbizi wa Syria walioko nchini Jordan kupitia Jumuiya ya utoaji misaada ya Hilali Nyekundu. Hussein Amir-Abdullahian amesema hayo alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan Nasser Jouder mjini Amman. Aidha kuhusiana na mgogoro wa Syria amesema kuwa, nchi za Magharibi na Marekani ndio wafadhili wakuu wa makundi ya kigaidi nchini Syria kwa sababu zinayapa silaha zinazotumiwa kuua watu na kuharibu miundombinu ya Syria.

Katika upande mwingine utawala wa Kizayuni wa Israel umepeleka makombora katika eneo la Haifa karibu na mpaka wa Syria, hatua ambayo imedaiwa na utawala huo kuwa ni jambo la kawaida. Hatua hiyo imechukuliwa siku kadhaa baada ya Jumuiya ya Kijeshi ya Nato kuweka mitambo ya makombora katika mpaka wa Uturuki na Syria, suala ambalo Damascus imelipinga na kusema ni uchokozi.

No comments: