Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, January 25, 2013

Harry: Niliua Waislamu ili nilinde Waingereza

Baada ya kurejea nchini kwake akitokea Afghanistan alikokwenda kuhudumu kwa kipindi cha miezi mitano, mrithi nambari tatu wa utawala wa Uingereza Prince Harry amesema kuwa aliua Waislamu ili kulinda watu wa taifa lake. Harry amesema alikuwa akiua watu huko Afghanistan kwa ajili eti ya kuokoa maisha ya watu wa Waingereza.
Hadi sasa haijabainika ni Waislamu wangapi wa Afghanistan waliouawa na mwanamfalme huyo wa Uingereza akitumia helikopta ya kijeshi ya Apache ambako amekutaja kuwa "kunamfurahisha" sawa kabisa na kuchezo mchezo wa video. Amesisitiza kuwa alifurahia kuua watu kwa kutumia helikopta kwa kuwa kitendo hicho kwake ni sawa na kucheza mchezo anaoupendelea wa video kwa kutumia PlayStation au Xbox.
Maelfu ya raia wasiokuwa na hatia wa Afghanistan wameuawa katika mashambulizi yanayoendelea kufanywa na majeshi ya nchi za Magharibi dhidi ya maeneo mbalimbali ya nchi hiyo.

No comments: