Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, January 25, 2013

A. Kusini: Majeshi ya Afrika yaongoze vita, Mali

Afrika Kusini imetangaza kuwa majeshi ya kigeni yanayopelekwa nchini Mali kwa ajili ya kupambana na makundi ya waasi wa kaskazini mwa nchi hiyo yanapaswa kuongozwa na nchi za Kiafrika.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini Ibrahim Ibrahim amesema kuwa operesheni ya majeshi ya kimataifa huko Mali inapaswa kuongozwa na Jumuiya ya Kiuchumi ya Magharibi mwa Afrika (ECOWAS).
Majeshi ya Ufaransa yalianza mashambulizi makali huko kaskazini mwa Mali Januari 11. Ufaransa ilichukua hatua hiyo kabla ya majeshi ya nchi za Kiafrika kuwasili Mali kwa ajili ya kushiriki mwenye operesheni ya kuwasaka waasi wa kaskazini mwa nchi hiyo wanaodhibiti miji kadhaa muhimu ya eneo hilo.

No comments: