Mshauri ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala ya
kimataifa amesema kuwa, Iran haitovumilia mashinikizo yoyote yale na
itachukua uamuzi kuhusiana na suala la nishati ya nyuklia bila ya
kuathirika na mashinikizo au vitisho. Ali Akbar Velayati amezungumzia
mashinikizo tarajiwa wakati huu wa kukaribia duru ijayo ya mazungumzo ya
Iran na kundi la 5+1 na kubainisha kwamba, Tehran itafanya mazungumzo
yajayo katika fremu ya sheria za kimataifa.
Velayati amesema, kutakuwa na matumaini ya kufikiwa natija katika mazungumzo yajayo ya Iran na 5+1 huko Baghdad endapo tu madola ya magharibi yataonyesha nia njema na kuweka kando utwishaji mambo usio wa kisheria. Inafaa kukumbusha hapa kuwa, duru ijayo ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran na kundi la 5+1 yanatarajiwa kufanyika hivi karibuni huko Baghdad, mji mkuu wa Iraq.
Velayati amesema, kutakuwa na matumaini ya kufikiwa natija katika mazungumzo yajayo ya Iran na 5+1 huko Baghdad endapo tu madola ya magharibi yataonyesha nia njema na kuweka kando utwishaji mambo usio wa kisheria. Inafaa kukumbusha hapa kuwa, duru ijayo ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran na kundi la 5+1 yanatarajiwa kufanyika hivi karibuni huko Baghdad, mji mkuu wa Iraq.
No comments:
Post a Comment