Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 15, 2016

Unicef: Watoto wakimbizi wanakabiliwa na hatari nchini Italia

Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (Unicef) umeeleza kuwa watoto wengi walionusurika kifo wakiwa katika safari ngumu kwenye bahari ya Mediterania wakitokea Libya kuelekea Italia hawakuongozana na watu wazima; na hivyo kuwafanya watoto hao kuwa katika mazingira ya kuweza kukabiliwa na vitendo vya unyanyasaji na kutumiwa kama watumwa.

Sarah Crowe, Msemaji wa Unicef amesema kuwa asilimia 92 ya watoto 7,600 ambao walivuka bahari ya Mediterania katika mazingira hatari kati ya Januari na Mei mwaka huu hawakuwa na wazazi au ndugu zao. Ameongeza kuwa wengi wa watoto hao walikuwa wavulana wenye umri kati ya miaka 15 na 17 kutoka Somalia, Nigeria na Eritrea.
Msemaji wa Unicef ametahadharisha kuwa wavulana na wasichana hao ambao waliwasili Ulaya wamekabiliwa na vitendo vya ukahaba, magenge ya udhalilishaji wa kijinsia na uhalifu. Itakumbukwa kuwa mwezi Februari mwaka huu wakala wa Umoja wa Ulaya wa Europol uliripoti kuwa watoto wakimbizi zaidi ya 10,000 ambao hawakuwa na wazazi au jamaa walipotea katika wimbi la wakimbizi la hivi karibuni kuelekea Ulaya.

No comments: